NA
RICHARD, KASHINJE 0764711129
rkashinje@gmail.com
MWALIMU
MWANAFUNZI
1 Mwalimu uwe makini, makini kumakinika
Mwalimu
si masikini, akilize kulabuka.
Walimu
sikilizeni, yamoyo yalotukuka
Mwalimu
ni mwanafunzi, kusoma hana kikomo.
2 Siku uwapo kazini, kusoma huna kikomo
Hata
kama nimezani, kitabu hakina komo
Pata
yawanazuoni, mapya kwako yaliyomo
Mwalimu
ni mwanafunzi, kusoma hana kikomo
3 Usishike mazoea, kusoma moja pekee
Kusema
umebobea, hakika si wapekee
Kazi
yako watachukua, waliosoma pekee
Mwalimu
ni mwanafunzi, kusoma hana kikomo
4 Usipokuwa msomi, tena wakusoma sana
Wanafunzi
hawakusomi, kwako ni aibu sana
Hawatakupenda
msomi, na hiyo fedheha sana
Mwalimu
ni mwanafunzi, kusoma hana kikomo
5 Kumbuka ile kauli, ambayo kwetu nirai
Mwalimu
kuwa mkali, wanafunzi kuzirai
Kwako
murua kauli, kwao somo wafurai
Mwalimu
ni mwanafunzi, kusoma hana kikomo
6 Siku zimebadilika, yakupasa utambue
Wanafunzi
huzunguka, ukweli wautambue
Yakupasa
kumakinika, wasomi wasiumbue
Mwalimu
ni mwanafunzi, kusoma hana kikomo.
7 Msomi tulikuamini, tuakukabidhi kazi
Kwakuwa
niutamaduni, nzuri ufanyapo kazi
Pia
tuanatatumaini, kazi iota mizizi
Mwalimu
ni mwanafunzi, kusoma hana kikomo
8 Kusoma hana kikomo, mwalimu ni
mwanafunzi
Mwanafunzi
hana komo, kusoma ni mwanafunzi
Haya
ndani yawe yamo, kazi ni uwanafunzi
Mwalimu
ni mwanafunzi, kusoma hana kikomo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni