Dhana
ya kategoria ya kisarufi ni dhana telezi na ina ukakasi katika kuieleza licha
ya uwepo wa wataalamu mbalimbali ambao
wamejaribu kuifasili. Katika kujibu swali hili tutaanza kueleza maana ya
kategoria jinsi ilivyoelezwa na wataalamu mbalimbali, tutaeleza maana ya
kategoria ya kisarufi, vilevile tutaelezea dhana ya sarufi mapokeo tukihusisha
mawazo ya wataalamu mbalimbali, pia
tutadadavua kategoria ya kisarufi kwa mkabala wa sarufi mapokeo hatimaye
tutahitimisha kwa kueleza faida na hasara za sarufi mapokeo.
Kwa
kuanza, tuijadili dhana ya kategoria ya kisarufi jinsi ilivyojadiliwa na
wataalamu mbalimbali kama ifuatavyo;
Zabroni (2013); anaeleza kuwa, kategoria
ni sifa zinazoambikwa katika aina mbalimbali za maneno.
Chombozi. Blogspot.com; waeleza
kuwa, kategoria ni aina za maneno kadri ya uainisho wake kutegemeana na sifa za
maneno husika kuwekwa katika kundi moja.
Matinde (2012); wanaeleza kuwa,
kategoria ni jumla ya maumbo, faridi na vipashio vilivyo katika hadhi sawa na huchangia sifa fulani katika tungo.
Hivyo, tunaweza kueleza kuwa
kategoria ni maumbo au vipashio mbalimbali vya kisarufi vinavyotumika
kubainisha mahusiano ya maneno katika tungo mbalimbali za lugha.
Baada ya kupata uelewa juu ya dhana
ya kategoria kama ilivyoelezwa na wataalamu mbalimbali, sasa tujadili dhana ya
kategoria ya kisarufi huku tukihusisha mawazo yetu na mawazo ya wataalamu mbalimbali kama ifuatavyo;
www.out.ac.tz;
wanaeleza kuwa, kategoria
ya kisarufi ni kundi la maneno lenye sifa za kisarufi zinazofanana.
Matinde (2012: 187); anaeleza kuwa, kategoria za kisarufi ni maumbo
au vipashio vya kisarufi vinavyotumika kubainisha mahusiano ya kategoria za
maneno katika sentensi.
www.
Englishclub.com; wanaeleza kuwa,
kategoria za kisarufi (grammatical category) inahusu sifa maalumu ya neno
ambayo inaweza kusababisha kwamba neno
au maneno kuhusiana
na mabadiliko katika mfumo wa kisarufi. ( tafsiri yetu)
www.thefreedictionary.com; wanaeleza kuwa,
kategoria za kisarufi ni aina za maneno yenye sifa za kisarufi zinazofanana.
Kwahiyo tunaweza
kusema kwamba, kategoria za kisarufi ni sifa ya kitu (maneno au neno) ndani ya
sarufi ya lugha.
Baada ya kueleza
maana ya kategoria ya kisarufi jinsi livyoelezwa na wataalamu mbalimbali na vyanzo
vingine. Sasa tuieleze dhana ya sarufi mapokeo huku tukihusisha mawazo ya wataalamu
mbalimbali kama ifuatavyo;
Massamba na wenzake (1999);
wanafafanua kuwa sarufi mapokeo ni sarufi elekezi ilisisitiza usahihi wa lugha
kwa kuonyesha sheria ambazo hazina budi kufuatwa, mathalani, kufanya muundo
fulani wa sentensi uonekana kuwa sahihi,
au sheria ambazo hazina budi kufuatwa
ili kufanya matamshi ya neno fulani yakubalike kuwa ndio sahihi. Sarufi hizo za kimapokeo zilikuwa zikisisitiza jinsi
ambavyo lugha haikupaswa kuwa.
Kwahali hiyo; tunaweza kusema kuwa,
sarufi mapokeo ni sarufi ya kale ambayo ilionekana kutokuwa na msimamo wa Kisayansi
katika kuelezea lugha bali ilikuwa na mwelekeo wa kifalsafa na kujikita katika
kutambulisha kategoria mbalimbali za kisarufi ambazo zinatumika hadi hivi sasa.
Baada ya kumaliza kujadili maana ya
sarufi mapokeo; sasa tuzigeukie
kategoria za kisarufi kwa mujibu wa mkabala wa sarufi mapokeo ,
Kategoria ya nafsi; hii ni kategoria
ya sarufi mapokeo ambayo huelezea viwakilishi vya matenda/ mtendwa ambavyo
huambikwa kwenye vitenzi.Jedwali lifuatalo linaoneshsa kategoria za nafsi tatu ambazo pia zinaonekana
katika maumbo ya umoja na wingi zikiwa na viambishi vipatanishi vyake.
Nafsi
|
Umoja
|
Viambishi vipatanishi
|
Wingi
|
Viambishi vipatanishi
|
I
|
Mimi
|
Ni-
|
Sisi
|
Tu -
|
II
|
Wewe
|
U -
|
Ninyi
|
M -
|
III
|
Yeye
|
A -
|
Wao
|
Wa -
|
Mfano wa utokeaji wa nafsi katika
tungo;
(i)
Ni-, hii huonesha nafsi ya kwanza .
Mfano; Mimi ninakula. (umoja)
Sisi tunakula. (wingi)
(ii)
U-,
hii
huonesha nafsi ya pili .
(iii)
Mfano:
Juma unakula? (umoja)
Juma mnakula? (wingi)
(iv)
A-, hii hueonesha nafsi ya tatu .
Mfano: Mtoto anakimbia. (umoja)
Watoto wanakimbia.
(wingi)
Kategoria ya njeo. ni kategoria ya kisarufi mapokeo
ambayo huonesha na kuelezea tendo linavyotendeka ,lilivyotendeka na litakavyotendeka.
Katika lugha ya Kiswahili kategoria za njeo huwakilishwa na viambishi vitatu
ambavyo ni; -na-, -li-, na –ta-.
(a) –na- katika kuonesha wakati uliopo
Mfano, Wanatembea.
Anakula.
(b) –li- hii huonesha wakati uliopita
Mfano, Watoto
walicheza mpira.
Walimu walifundisha.
(c) -ta- hii huonesha wakati ujao
katika tungo.
Mfano, Mwalimu atafundisha kesho.
Rehema atarudi wiki ijayo.
Kategoria ya idadi. Hii ni kategora ya sarufi mapokeo
ambayo huonesha idadi katika tungo zinazohusu umoja na wingi. Mara nyingi
huonekana katika nomino na aina zingine za maneno kama vile vitenzi na vivumishi.
Mfano.
(a)
Mtoto anakimbia.
(umoja)
Watoto wanakimbia . (wingi)
(b)
Msichana mzuri . (umoja)
Wasichana wazuri.
(wingi)
Kwa kurejerea mifano hii
viambishi m- na wa-
kwa pamoja ni kategoria za idadi.
Kategoria ya hali. Hii ni kategoria ya kisarufi
mapokeo ambayo huelezea utendekaji wa
lile tendo ambalo lawezakuwa katika hali timilifu yenye kiambishi -me-
au hali ya mazoea yenye kiambishi hu-
Mfano; -me- katika hali timilifu
(a) Mwanaidi ametoroka nyumbani.
(b) Mwalimu amefundisha kiswahili.
(c) Juma amekimbia kichakani.
Mfano; hu-
katika hali ya mazoea
(a) Mutta hufundisha Kiswahili.
(b) Tababa hutembea harakaharaka.
Kategoria ya jinsia; hii ni aina ya kategoria ya kisarufi
mapokeo ambayo hubainisha maumbile katika tungo. Zipo jinsia za aina mbili.
(a) Jinsia ya kibaiolojia
(b) Jinsia ya kisarufi
(a) Jinsia ya kibaiolojia; hii ni aina
ya jinsia inayohusu maumbile ya mtu .Aina
hii husawiriwa na lugha. Aidha katika
lugha ya Kiingereza maneno kama Patron, He, Boy na Headmaster hudokeza jinsia
ya kiume ilhali yale ya Matron, She, Girl na Headmistress hudokeza jinsi ya
kike.
(b) Jinsia ya kisarufi; udhihilishwa na
maneno ya augha kuwekwa kwenye makundi bila kuzingatia kigezo cha kibaiolojia.
Hata hivyo, baadhi ya nomino katika lugha ya Kiswahili mfano; msichana,
mvulana, bibi, Baba , mama, kaka, dada na babu hudokeza jinsia.
Kategoria ya dhamira. Mtei (2008
uk.140); anaeleza kategoria ya dhamira na kuanza na fasili ya dhamira kuwa ni
kipengere cha kisarufi na kimaana ambacho huonesha lengo/ maana/
mwelekeo inayoiburiwa na vitenzi mbalimbali katika sentensi. Baada ya fasili
hii amabainisha aina za dhamira kama ifuatavyo;
(a) Dhamira elezi/ arifu; hii hutumiwa kueleza ukweli wa mambo jinsi ulivyo
vilevile hutoa taarifa kuhusu jambo.
Mfano, (i)
Mzozo huu umetatuliwa.
(ii) Mwizi yule alikamatwa.
(b) Dhamira amrishi; anaieleza kuwa
nidhamira ambayo hutumiwa kuonesha amri, ombi/ kutahadharisha.
Mfano, (i)
Simama juu.
(ii) Lete hilo jembe.
© Dhamira tegemezi; hii hutumiwa
kuonesha hali ya kutokuwa na hakika au uwezekano wa mambo au kutokea kwa matukio
.
Mfano,
(i) kutokuwa na hakika.
(a) Labda hakupata taarifa zako.
(b) Ikiwezekana nitakuja nae.
(ii) kutegemea kwa matukio.
Mfano,
(a) Mwalimu angenipa mtihani wangu
ningeweza kufanya masahihisho.
(b) Shule zikiongezeka watoto wengi watapata
elimu.
(iii) uwezekano wa jambo.
Mfano, (a) Mvua ingenyesha asubuhi tu.
(b) uzembe wake ungedhibitiwa
mapema.
Kategoria
ya kauli; katika kufafanua dhana hii Matinde (2012:190-205) anaeleza dhana ya
kauli kuwa, ni kategoria ya kisarufi ambayo uamilifu wake umekitwa katika kitenzi. Pia amezibainisha kauli mbalimbali
zinazojitokeza katika lugha ya Kiswahili kama ifuatavyo;
I.
Kauli ya kutendwa; hii ni kauli ambayo hubainisha kuwa kiima ni mtendewa au
mtendwa.
Mfano, (i) Uwanja umefyekwa.
(ii) Nyumba
imechomwa.
II.
Kauli tendi; hii ni kauli ambayo
hubainisha kuwa kiima ni mtenda. Kauli hii
huonyesha kuwa nomino iliyopo kwenye kiima ndiyo; ilitenda, itatenda, au
inatenda kitendo husika katika tungo.
Mfano.
(i) Mwajuma alipanda maboga.
(ii)
Mwalimu anafundisha.
III. Kauli ya kutendeka; hii haioneshi
uhusiano ulio wazi baina ya kiima na yambwa. Hata hivyo, kiima hupata
athari kutokana na kitendo husika. Katika kauli hii alomofu zinazoonesha kauli
hii ni {-ik-}, {-ek-}, {-lik-}, {-lek-}, {-ikan-} na {-eken-}.
Mfano,
(i) Nyumba inaanguka.
(ii) Kiti kimevunjika.
(iii) Fanyika
(iv) Vukika
(v) Tosheka
(vii) Ngoma hiyo haikututeka.
V.
Kauli ya kutendewa; hii hujumuisha
vitenzi vinavyotokana na kauli ya kutendea kuongezewa viambishi. Alomofu zake
ni {–w-}, {-liw-}, {-iw-} au {-ew-}
Mfano,
(i) Pigwa
(ii) Cholewa
(iii) Imbiwa
VI.
Kauli ya kutendeka; hii ni kauli ambayo
huonesha jinsi jambo linavyotendeka. Alomofu zinazobainishwa katika kauli hii
ni {-ek-}, {-ik-}, {-lik-}
{-elek-}, {-ikan-}, na {-iken-}.
Mfano; (i) pigika
(ii) chezeka
(iii) Someka
VII.
Kauli ya kutendua; kauli hii
hudhihirishwa na kinyume cha utenduzi. Alomofu za kauli hii ni. {-u-}, {-a-},
{-i}, {-e-}.
Mfano: (i) Fungua
(Ii) Umbua
(Iii) Chomoa
VIII. Kauli
ya kutendana; hii ni kauli ambayo hubainisha
uhusiano fulani kati ya kiima na yambwa. Alomofu za kauli hii ni {-an-}
Mfano.
(i) Sukana
(ii) Chekana
(iii) Somana
IX.
Kauli ya kutendesha; hii ni kauli ambayo
hubainisha dhana ya usababisho kati ya kiima na yambwa. Alomofu zinazojitokeza
katika kauli hii ni: {-esh-}, {-lesh-}, {-lish}, {-ez-}, {-iz-} ambazo
hutegemea vitenzi husika katika tungo.
Mfano; (i) Ogesha
(ii) Pigisha
(iii) Chezesha
Kategoria ya uhusika;
Matinde (2012:207), ameeleza uhusika kuwa ni kategoria ya kisarufi ambayo
huonyesha uhusiano wa viambajengo katika tungo. Aidha huonyesha uamilifu wa
kila kiambajengo katika tungo na athari ya kila kiambajengo hicho kwa
viambajengo vingine. Uhusika huu huweza kugawanyika katika aina sita kama
ifuatavyo;
(i)
Uhusika wa kiima; huu hubainisha kuwa
nomino, au kiwakilishi chake huchukua nafasi ya kiima.
Mfano: (a) Daktari
alimkaribisha mgonjwa.
(b) Musa
amejengewa nyumba .
(ii) Uhusika
tendea; uhusika huu huonyesha kuwa nomino au kiwakilishi chake kinathirika kutokana na tendo fulani.
Mfano: (a) Mwiba
ulimchoma Jeska.
(b) Yeye alifukuzwa na mwalimu.
(iii)
Uhusika ala; huu huonesha kitu ambacho hakina hisia kilichotumika katika kutekeleza kitendo au jambo fulani.
Kifaa hiki hutumika kusababisha utokeaji wa tendo au hali ambayo inadokezwa na
kitenzi.
Mfano: (a)
Alivunja mlango kwa nyundo.
(b) Alimkata kwa panga.
(iv)
Uhusika yambwa; huu huonyesha kuwa nomino au kiwakilishi chake kimechukua
nafasi ya yambwa katika tungo.
Mfano: (a) Jumanne alinunuliwa baisikeli.
(a)
Mfano: Mwanafunzi aliyefauru vizuri
awazawdiwa daftari.
(v)
Uhusika mahali; huu hubainisha mahali au mwelekeo wa kieneo wa hali au tendo
ambalo linadokezwa na kitenzi.
Mfano: (a) Mbwa yuko nyuma ya kabati.
(b) Ameweka jagi chini ya meza.
(vi)
Uhusika mtendwa au mtendewa; huu
hudhihirisha kiumbe chenye hisia ambacho kinathirika na hali au tendo
linalodokezwa na kitenzi.
Mfano: (a) Mtoto aliangushwa naa mbuzi wake.
(b) Yule msichana amechomwa na mwiba.
Kategoria ya ngeli;
Wahiga (1999:40), analeza maana ya ngeli kuwa ni jamii ya nomino zenye kuleta
mabadiliko ya aina moja ya viambishi vya maneno katika umbo la umoja na wingi. Masebo
na wenzake (2003) wanaeleza kuwa, huu ni mtazamo mkongwe zaidi uliofuatwa na
wanasarufi mapokeo ambao miangoni mwao alikuwa ni Meinholf baadaye akafuatwa na
Broomfeld (1931) na Ashitoni (1944) ambao waliziainisha nomino kulingana na
viambishi awali vya nomino. Nomino zote zilizokuwa na viambishi vinavyofanana
ziliwekwa katika kundi moja na kufanya ngeli moja.
Mfano
ni katika jedwali lifuatalo;
|
Ngeli
|
Viambishi
awali vipatanishi
|
Mifano
|
1
|
A-WA
|
A- Umoja
WA-
wingi
|
Mtoto
anakuja - watoto wanakuja
Mwalimu
ameondoka - walimu wameondoka
|
2
|
U-I
|
U-
umoja
I-wingi
|
Mmea
umenyauka - mimea imenyauka
Mkungu
umenunuliwa - mikungu imenunuliwa
|
3
|
LI-YA
|
LI-Umoja
YA-
wingi
|
Yai
limepasuka - mayai yamepasuka
Embe
limeoza - maembe yameoza
|
4
|
KI-VI
|
KI-
Umoja
VI-
Wingi
|
Kiti
kimevunjika - viti vimevunjika
Kikombe
kimekatika - vikombe vimekatika
|
5
|
I-ZI
|
I-umoja
ZI-
wingi
|
Nyanya
imechumwa - nyanya zimechumwa
Soda
imeuzwa - soda zimeuzwa
|
6
|
U-ZI
|
U-
umoja
ZI-wingi
|
Ufunguo
umepotea - funguo zimepotea.
Uzi
umenunuliwa - nyuzi zimenunuliwa.
|
7
|
U-YA
|
U-
Umoja
YA-
wingi
|
Ugonjwa
umeenea - magonjwa yameenea
Uasi
umeisha - maasi yameisha
|
8
|
KU
|
KU-
Umoja
|
Kusuka
kunachosha
Kuigiza
kunaburudisha
|
9
|
PA-MU-KU
|
PA-umoja
MU-Umoja
KU-
umoja
|
PA-
Mahali hapa pananuka
MU-
Mahali humu munamaji
KU-
Mahali kule kuna giza.
|
Kwa
hiyo, licha ya wanasarufi mapokeo kutumia lugha ya kilatini kama kigezo cha
kupima ubora wa lugha kuwa ni makosa kwa sababu ya kuwa kila lugha ina mtindo
wa kipekee wa kuunda tungo zake, lakini faida kubwa inayojitokeza kwa
wanasarufi mapokeo ni kuwa waliweza kuanzisha kategoria mbalimbali za kisarufi
ambazo zinatumika mpaka sasa katika uga wa sarufi.
MAREJELEO
Masebo na wenzake, (2002). Kiswahili
Kidato cha 3 na 4. Nyambari Nyangwine Publishers:
Dar es Salaam.
Massamba na wenzake, (1999). Sarufi Miundo ya Kiswahili Sanifu (SAMIKISA). TUKI:
Dar es Salaam.
Matei, A. K. (2008). Darubini ya Sarufi. Phoenix Publishers: Nairobi.
Matinde, R. S. (2012). Dafina ya Lugha; Isimu na Nadharia. Serengeti Educational
Publishers
(T)
Limited: Mwanza.
Philipo, Z. (2013). Sintaksia ya Kiswahili. Chuo Kikuu cha Dodoma: Dodoma.
Waihiga, G. (1999). Sarufi Fafanuzi ya Kiswahili. Longhorn Publishers: Nairobi.
www.chombozi.blogspot.com.
(Ilitembelewa tarehe 23/12/2014 saa 04:30 usiku.)
www.englishclub.com.
(Ilitembelewa tarehe 23/12/2014 saa 05:45 usiku.)
www.out.ac.tz.
(Ilitembelewa tarehe 23/12/2014 saa 05:50 usiku.)
www.thefreedictionary.com.
(Ilitembelewa tarehe 24/12/2014 saa 07:01 usiku.)
Inapendeza sana na inasaidia kuongeza ufahamu.HONGERA
JibuFutaASANTE KAKA
JibuFutaswali.jadili ni kwa nini hamna lugha bora wala duni?
JibuFutaKilonzi Enoch, ni kweli hakuna lugha bora wala duni kwasababu kuu mbili: kwanza, kila lugha ina sifa ya kujitosheleza kimatumizi. Wazungumzaji wa (tuseme) lugha ya kimasai hukamilisha mawasiliano yao bila msaada wa lugha "bora" yoyote. Pili,Lugha yoyote huweza kuwa na hadhi kubwa kutegemea hali ya kiuchumi, kisiasa,na kiteknolojia. Kwa mfano lugha ya Kiingereza INA hadhi kubwa kutokana na sababu za kihistoria za wazungumzaji wake - wazawa.
FutaNb: lugha yenye hadhi kubwa ni ile ambayo imekua kimatumizi eneo kubwa la kijiografia, huwa na kamusi, hutumika maeneo mengi rasmi, huwa na sarufi ambayo hufundishwa shuleni, nk lakini haya yote ni mambo ya ziada sana. Jambo la msingi katika lugha ni kukamilisha mawasiliano katika jamii fulani sifa ambayo lugha yoyote inayo.
Tafadhali naomba outline :Kwa kutumia nadharia ya sarufi mapokeo, eleza mambo makuu matatu wanayosisitiza kuhusu sintaksia ya lugha na Kisha toa maoni yako kwa kuzingatia wakati huo wa Enzi za mapokeo na wakati wawakati wa sasa
JibuFutaNisaidie aina za maneno kwa mtazamo wa kimuundo
JibuFutaSwali:
JibuFuta1. Jadili Kategoria za kisarufi
a). Kimuundo
b). Toa ushahidi wa kuwepo kwa kategoria hizo katika lugha
Kelvin Mwasikili
FutaKazi nzuri nimepata maarifa mapya. Tunaomba ungetuma na ushahidi wa kuwepo Kwa kategoria za kileksika
JibuFutaJadili ubora wa sarufi elekezi
JibuFutaNaomba utuelezee kategoria za kileksika kwa mifano
JibuFutawiniely
Futanaomb ufafanuzi juu ya Kaategoria ya jenda/ jinsia ma aina za kategoria hiyo
JibuFutaUdhaifu wa makabala wa kimapokeo niupi?
JibuFutaUmechambua vizurii kategoria za kisntksia kwa mkbla wa kimapokeo
JibuFutaUmechambua vizurii kategoria za kisntksia kwa mkbla wa kimapokeo
JibuFutaDhihirisha mitazamo mitatu ya kikategoria kwa kina kisha toa maoni juu ya mtazamo faafu. Naomba nisaidie ili swali
JibuFutaudhaifu wa wanasarufi mapokeo ndio chanzo cha sarufi za kisasa.jadili
JibuFutaKibona v.
FutaShukrani Sana hakika nimeongeza nashida mapya
JibuFutaKazi nzuri hongera sana
JibuFutaKazi njema...
JibuFutaHongera. nina swali
JibuFutaZikague sentensi Kisha uyajibu maswali yanayofuata.
1.juma amelala
2.juma alimpiga hamisi
3.juma alimpikia hamisi chakula
4.wanafunzi humchaguaHamisi kiranja wao kila mwaka.
Maswali
1.kwa kila mojawapo ya sentensi hizo. Yaainishe maneno yaliyotumiwa katika Kategoria za kisarufi.
2.uainishe muundo WA kila sentensi ukizingatia uamili WA maneno uliotumika.
3.kwa kila sentensi chora kielelezo matawi.
asante sana nimeweza kuongeza ufahamu.
JibuFutaHongera umefanya kazi nzuri sana
JibuFutaNimeelewa Sana hongera
JibuFutaAhsante sana nimepanua wigo wa ufahamu juu ya sintaksia
JibuFutaNakala ipo vizuri hivyo ni vyema kwa mtunzi kuiendeleza haiba yake ya utunzi hata katika mawanda mengine ya kisarufi Kama vile wanamuundo.
JibuFuta