RICHARD, KASHINJE NDIYE MWANZILISHI NA MWANDISHI WA BLOG HII
HISTORIA YA TAFSIRI
Historia
na maendeleo ya tafsiri ulimwenguni imeelezwa na wataalamu mbalimbali ambao ni
kama vile Mwansoko na wenzake (2006), Wanjala (2011), Mshindo (2010), Sofer
(2006) ambapo wataalamu hawa wamegawa historia na maendeleo ya tafsiri katika
vipindi vifuatavyo:
Enzi za kale. Kipindi hiki kinajumuisha wakati
wote wa kihistoria kati ya mwaka 300KK hadi 300BK. Hiki ni kipindi ambacho
kilikuwa na maendeleo ya sayansi na taaluma nyingi za kisasa ambapo
zinasadikika zilianzia huko Misri. Ugunduzi na ustaarabu ulioletwa na wamisri
uliigwa na wayunani na kuwa chimbuko la ustaarabu wa ulaya. Mbinu iliyotumika
na wayunani kuchota maarifa ya wamisri ni tafsiri. Wayunani walikaa misri kwa
muda na kujifunza lugha ya wamisri na elimu yao. Mambo waliojifunza
waliyafasiri kwa kiyunani na kwenda kuyasambaza huko ulaya.
Enzi za giza. Hiki ni kipindi kati ya karne ya 5
hadi 11. Kipindi hiki kiliitwa kipindi cha giza kwasababu kilitawaliwa na
misingi ya utamaduni kuoza na uozo wa kijamii kukita mizizi ambapo mambo kama
ubashi, ukahaba na unajisi vilikithiri, pia shughuli za elimu zilikwama huko
ulaya. Katika kipindi hiki kulikuwa na mapigano kati ya waislamu na wakristo
ambapo baada ya mapigano hayo maarifa ya wagiriki yaliyosheheni ujuzi wa
sayansi yalifasiriwa kwa kiarabu. Pia baadhi ya mataifa mfano Hispania
yalichukua vitabu ambapo vilikuwa vimesheni maarifa ya sayansi na kuyapeleka
kwao na kutafsiri katika lugha zao. Tafsiri hizo zilipelekea ulaya kutoka
katika kipindi cha giza na kuingia katika kipindi cha ufufuko wa elimu na maarifa.
(Renaissance)
Enzi za ufufuko. (Renaissance) inamaana ya ufufuko wa hamu kuu ya
elimu na maarifa. Kipindi hiki kilivuma sana ulaya kusini hasa Italia kikiwa na
lengo la kufufua shughuli za elimu na utamaduni. Wazungu walipofika Uarabuni
walistaajabia elimu ya kisayansi wakayachukua maarifa hayo na kuyafasiri katika
lugha mbalimbali mfano kifaransa, kijerumani na kiingereza. Fasili hizo zilizua
msisimko wa shughuli za kielimu, maarifa na utamaduni.
Enzi za kati. Hiki ni kipindi kilichoonesha muamko
wa kidini katika karne ya 16 ambapo ilianza ujerumani na kusambaa katika maeneo
mengine ulimwenguni. Mwamko huu ulipinga muundo, mwelekeo, falsafa na mafunzo
mengi ya kanisa katoliki ya wakati huo na matumizi ya lugha moja ya kilatini
katika misa na mafunzo. Hali hii ilisababisha mgawanyiko katika dini ya
kikristo, watu mbalimbali walitafsiri maandiko matakatifu katika lugha
mbalimbali kwa mfano Martin Luther King alitafsiri biblia takatifu kutoka
kilatini kwenda kiingereza (1611) ikaitwa The King James Bible, pia alitafsiri
biblia kutoka kilatini kwenda lugha ya kijerumani. Baada ya kuona tafsiri ya
kilatini imeacha baadhi ya vipengele katika maandiko hayo matakatifu . Jarome
alitafsiri biblia ya kigiriki na kiebrania kutoka kwenye lugha ya kilatini
Enzi za kisasa. Kipindi hiki kilikuwepo karne ya 20
ambapo kilijulikana kama kipindi cha tafsiri kutokana na wingi au mfumuko wa
tafsiri. Kipindi hiki kimetawaliwa na masafa marefu ya mawasiliano, maendeleo
makubwa ya kielimu na ethnolojia, utandawazi na usomi wa lugha, isimu na
fasihi. Mikataba ya kimataifa baina ya mashirika ya umma na ya binafsi
inafasiriwa kwa yeyote anayehitaji taarifa hizo. Tafsiri ilikolea katika karne
hii kutokana na kuzuka kwa mataifa mengi huru yanayoteua lugha rasmi, lugha za
taifa na lugha za elimu.
Kwa
hiyo baada ya hitaji kubwa la watu kutaka kuwasiliana na jamii au watu wa
mataifa, kabila tofauti. Kutokana na hitaji lake kubwa hilo imepelekea taaluma
hii kukuwa kwa kasi sana ukilinganisha kipindi cha nyuma hasa baada ya mapinduzi ya viwanda karne ya
18.
Baada
ya kujadili historia na mandeleo ya tafsiri ulimwenguni, sasa tunaweza kujadili
historia na maendeleo ya tafsiri nchini Tanzania.
Kwa
ujumla historia na maendeleo ya tafsiri nchini Tanzania haina historia ndefu
sana kwani inaanzia mnamo karne ya 19 ambapo tunaweza kugawa historia na
maendeleo haya katika vipindi vitatu ambavyo, ni kabla ya utawala wa kikoloni,
wakati wa utawala wa kikoloni na baada ya uhuru.
Kabla ya utawala wa kikoloni, wamisionari walitafsiri vitabu
mbalimbali vya kikristo ikiwemo biblia takatifu kutoka lugha ya
kiingereza kwenda Kiswahili na lugha nyingine za makabila kwa lengo la kueneza
dini na ustaarabu wa kikristo kwa waafrika.
Wakati wa utawala wa kikoloni, hiki ni kipindi kuanzia miaka ya
1800, katika kipindi hiki wakoloni hasa waingereza walitafsiri maandiko
mbalimbali ya kitaaluma na fasihi ya Ulaya kwa lugha ya Kiswahili. Mfano Pia
kabla ya uhuru baadhi ya kazi za fasihi zilitafsiriwa kwa mfano tamthiliya ya Mzimu wa Watu wa Kale
iliyotafsiriwa na Mohamed S. Abdalla
(1960) kutoka lugha ya kiingereza (Shrine of The Ancestors).
Baada ya uhuru ambayo ni kuanzia
mwaka 1961, katika
kipindi hiki wapo wataalamu waliofanya juhudi za kutafsiri vitabu mbalimbali
kwa lugha ya Kiswahili mfano mzuri ni Mwalimu Julius K. Nyerere ambaye
alitafsiri vitabu viwili vya mwandishi mashuhuri wa tamthiliya wa huko
Uingereza William Shakespeare ambavyo ni tamthiliya ya Juliasi Kaizari (Julius
Caesar) (1963) na tamthiliya ya Mabepari wa Venis (The Merchant of Venis)
(1969).
Kazi nyingine zilizotafsiriwa baada
ya ukoloni ni pamoja na ushairi wa Wimbo
wa Lawino iliyotafsiriwa na Paul Sozigwa (1975), kutoka lugha ya kiingereza
(Song of Lawino), riwaya ya Uhuru wa Watumwa iliyotafsiriwa na East African Literature Bureau (1967) kutoka lugha ya kiingereza (The Freeing of The Slaves in East Africa).
Pia kazi nyingine za fasihi ambazo zimetafasiriwa kwa lugha ya Kiswahili hapa
Tanzania ni pamoja na Nitaolewa
Nikipenda ambacho kimetafsiriwa na Crement M. Kabugi (1982) kutoka lugha ya
kiingereza (I will marry when I Want).
Kwa
sasa maendeleo ya taaluma ya tafsiri nchini Tanzania yamepiga hatua kubwa
kutokana na kukua kwa sayansi na teknolojia. Taaluma ya tafsiri kwa sasa
inafundishwa katika elimu ya sekondari na vyuo mbalimbali. Pia taasisi na asasi
zinazojishughulisha na tafsiri zimeongezeka kwa mfano Baraza la Kiswahili la
Zanzibar (BAKIZA), Taasisi ya Kiswahili na Lugha za Kigeni (TAKILUKI), Baraza
la Kiswahili la Taifa (BAKITA), Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI) na
NADHARIA
MAHUSUSI ZA TAFSIRI.
1. Nadharia ya Usawe wa Kimuundo; nadharia hii inatetewa na mtaalam
Catford (1969), Tunapofanya kazi ya kutafsiri tunatakiwa kuzingatia ulinganifu
wa kimuundo kati ya matini chanzi na matini lengwa, maana yake ni kwamba muundo
wa matini chanzi ujitokeze katika matini lengwa. katika nadharia hii muundo ni
muhimu. Pia nadharia hii hutumika zaidi katika kutafsiri maandiko ya kidini
hasa Biblia.
2. Nadharia ya Usawe wa Kidhima; wa tetezi wa nadharia hii ni pamoja
na Nida (1964) na Nida na Taber (1969) wanaona kuwa usawe wa kidhima ni muhimu zaidi
kuliko usawe wa kimuundo. Wafasiri wanapaswa kuhakikisha kwamba dhima ya matini
chanzi pamoja na athari zake zinajitokeza katika matini lengwa. Yaani kama
matini chanzi inawalenga watoto inapaswa iandikwe kiasi kwamba watoto wataweza
kuelewa. Pia kwa kuzingatia nadharia hii unapaswa kutumia lugha rahisi na
inayoeleweka na watu wote. Vilevile tafsiri yako iwe nzuri kiasi kwamba mtu
atakaposoma asiweze kujua kwamba hii kazi imetafsiriwa.
3. Nadharia ya Usawe wa Aina-matini; matini yoyote ile ifasiriwe kwa
kuzingatia aina yake. Hii inamaana kwamba kazi itakayotokea itafanana na matini
chanzi. Kma matini chanzi ni ya kisheria itakapotafsiriwa matini lengwa nayo
itaonekana kuwa ya kisheria. Katika nadharia hii kinachozingatiwa ni fani
(muundo) na maudhui (dhima/lengo) ya matini yenyewe inayotafsiriwa. Watetezi wa
nadharia hii ni Reiss (1971), Buhler (1965) na Newmark (1982/88)
4. Nadharia Changamani (Cross
Fertilization theory).
Hii ni nadharia tete iliyoasisiwa na P.S.Malangwa (2010) Ndharia hii inadai kwamba
huwezi kufanya tafsiri kwa kutumia nadharia moja tu, kwa sababu hakuna nadharia
inayojitosheleza yenyewe.
UAINISHAJI WA MTINI
Maana:
Kuainisha matini ni kuzigawa au kuziweka matini katika makundi mbalimbali kwa
kuzingatia kufanana kwake. Sababu: Tunaainisha matini kwa sababu kila matini
inahitaji mbinu maalum ya kuitafsiri. Mikabala/vigezo vya uainishaji: Wataalam
wengi wanatumia vigezo vitatu ambavyo ni Kigezo cha Mada (Topic/Field), Kigezo
cha Matumizi ya Istilahi, Kigezo cha Dhima kuu za Lugha
1. Kigezo cha Mada: katika kigezo hiki tunaangalia
maudhui ya jumla ya matini. Tunajiuliza matini hii inahusu uwanja gani hasa
katika maisha? Kwa kutumia kigezo hiki cha mada tunapata aina tatu za matini.
i) Matini za Kifasihi (Literary Text); hizi ni matini ambazo zinahusu fani
mbalimbali za fasihi kama vile riwaya, tamthilia, ushairi nk. ii) Matini za
Kiasasi (Institutional Texts); matini hizi ni mtini za kimamlaka kama vile
matini za kisiasa na kiserikali (hotuba, risala, mikataba, vyeti nk). iii) Matini
za Kisayansi (Scientific Texts); matini hizi hujumuisha masuala yote ya Sayansi
na Teknolojia. Kwa mfano; Fizikia, Kemia, Biolojia nk.
2. Kigezo cha matumizi ya Istilahi: katika kigezo hiki kinachozingatiwa
hapa ni kwamba, matini huainishwa kwa kuangalia wingi au idadi za
istilahi-msamiati wa uwanja maalum/husika mf: sharia nk. Kwa kutumia kigezo
hiki tunapata aina tatu za matini:
a) Matini za kiufundi (Technical Text), matini
hizi huwa na idadi kubwa ya istilahi.
b) Matini za kinusu ufundi (Semi-Techinical
Text), matini hizi huwa na idadi ndogo au chache za istilahi.
c) Matini za zisizo za kiufundi (Non
Techinical Text), matini hizi ni zile ambazo hazina kabisa istilahi bali
hutumia maneno ya kawaida kabisa.
3. Kigezo cha Dhima Kuu za Lugha
(Major Language Functions).
Buhler (1965) alipendekeza dhima kuu 3 za lugha.
i)
Dhima elezi (Expressive Function), katika dhima hii lugha hutumika kuelezea
hisia za mwandishi/mzungumzaji. Anasema, mzungumzaji au mwandishi hueleza hisia
zake bila kumjali msikilizaji au msomaji.
ii)
Dhima Arifu (Informative Function), dhima hii ya lugha hujitokeza pale ambapo
matini au lugha inatumika katika kutoa taarifa kuhusu jambo fulani. Dhima hii
huegemea kwenye ukweli wa mambo.
iii)
Dhima amili (Persuasive Function) katika dhima hii lugha hutumika kuchochea
hisia za msikilizaji au msomaji. Kiini cha dhima hii ni hadhira. Kwa hiyo, kwa
kuzingatia dhima hizi tatu “3” tunapata aina kuu tatu za matini kama ifuatavyo:
1. Matini Elezi (Expressive Texts);
matini hizi huegemea upande wa mwandishi. Mwandishi hutumia matini hizi
kuelezea hisia zake. Mfano, kazi mbalimbali za kifasihi, hotuba, matini
mbalimbali za kimamlaka, matini za kisheria, matini mbalimbali za kitaaluma,
maandishi binafsi nk. 2.
2. Matini Arifu (informative Texts); matini hizi
ni zile ambazo zinatoa taarifa au maarifa kuhusu jambo fulani. Sifa yake ni
kuwa zinakuwa na umbo sanifu au umbo maalum mfano; umbo la jarida, kitabu,
ripoti, tasnifu, vitabu vya taaluma mbalimbali nk. 3. Matini Amili (Persuasive
Texts); matini hizi huegemea upande wa hadhira. Katika matini Amili mwandishi
hujitahidi kadiri awezavyo kuchochea hisia za wasomaji na kuwafanya watende
kama ambavyo mwandishi anataka watende. Hivyo huegemea upande wa msomaji. Mfano
wa matini hizo ni kama vile mialiko mbalimbali, matangazo, maelekezo mbalimbali
nk.
UCHAMBUZI
WA MATINI ZA TAFSIRI
Awali
ya yote mchambuzi wa matini za tafsiri/mfasiri anapaswa kusoma matini kwa kina
na kuyaelewa kabla ya kuanza zoezi zima la uchambuzi wa matini. Maana:
Uchambuzi wa matini unatuwezesha kubaini sifa na vipengele vinavyojenga matini
husika kimuundo, kidhima na kiitikadi. Hatua/vipengele vya uchambuzi wa matini:
Uchambuzi wa matini unahatua tatu “3” ambazo ni kama ifuatavyo:
1.
Kusoma matini yote na kuielewa vizuri. Hii humsaidia mfasiri kuweza kuandaa
marejeleo muafaka, kuandaa vitabu au machapisho mbalimbali yatayomsaidia katika
zoezi zima la kufasiri matini. Kwa mfano; - Kuandaa kamusi mbalimbali kama vile
kamusi ya lugha chanzi, kamusi ya lugha lengwa, kamusi ya visawe, kamusi ya
fani maalum. - Inamsaidia mfasiri kuandaa orodha ya istilahi. - Inamsaidia
mfasiri kuweza kugawana sehemu au vipengele vya matini kwa wafasiri wengine.
2.
Kuchambua matini yenyewe. Uchambuzi wa matini hulenga kupata nduni bainifu za
matini husika (Distinctive Features). Kipengele hiki cha pili kina hatua ndogo
ndogo tano ambazo ni kama ifuatavyo:
a) Kubaini lengo la mwandishi wa matini
chanzi. Mfano; malengo ya mwandishi huweza kuwa kukweza, kusifu, kukashfu au
kuarifu jambo. Kwa kawaida waandishi wa matini chanzi wanakuwa na mitazamo
mitatu;
i)
Mtazamo hasi kwa mtendwa (biased) mfano, katika gazeti; “Chelsea yaichabanga
Arsenal tatu nunge”
ii)Mtazamo
chanya kwa mtendwa (biased) mfano katika gazeti; “Chelsea yafuta uteja kwa
Arsenal”
iii) Mtazamo wa kati (neutral) mfano katika
gazeti; “Chelsea yaifunga Arsenal au Arsenal yafungwa na Chelsea”
b) Kubaini lengo la mfasiri. Mfasiri anapaswa
kujiuliza kwa nini nafasiri kazi hii? Je lengo langu na mimi ni tofauti na la
mwandishi? - Aepuke upendeleo kwa hadhira chanzi na hadhira lengwa badala yake
ajikite katika ukweli. Hivyo inafaa awe katika mtazamo wa kati (neutral) - Kama
kuna haja ya kuegemea upande mmoja basi aegemee kwa hadhira lengwa.
c) Kubaini hadhira na umbo la matini. Kwa
mfano; kama matini chanzi ni kitabu basi matini lengwa nayo iwe kitabu.
d) Kubaini mtindo wa matini. Hapa mfasiri
ahakikishe kwamba mtindo wa matini chanzi unajitokeza katika matini lengwa.
Mfano; kama kuna monolojia au dayalojia basi na matini lengwa inapaswa kuwa
hivyo.
e) Kubaini ubora na mamlaka ya matini chanzi.
Hapa mfasiri hanabudi kuzingatia ujuzi wa mwandishi katika kutumia zana za
kiisimu/vipengele mbalimbali vya lugha. Mamlaka hutokana na hadhi au ubobevu wa
mwandishi huyo katika taaluma au fani aliyoandikia. Mfano, kazi ya fasihi ya S.
Robert ni bora kuliko iliyoandikwa na mimi kwa sababu yeye ni mbobevu/galacha katika
taaluma hiyo.
3.
Kusoma matini kwa mara ya mwisho. Katika hatua hii ya tatu mfasiri asome tena
matini chanzi ili kutoa taashira (highlight) kuhusu maneno au mambo muhimu.
Mambo muhimu ni: Majina mahususi ya watu, mahali, sehemu au miaka, maeneo ambayo
hayatafsiriki kirahisi ili aweze kuyashughulikia upya hapo baadaye.
MCHAKATO WA KUTAFSIRI/KUFASIRI
Hatua
muhimu katika kutafsiri Tunapofanya tafsiri kuna hatua muhimu kuu sita kwa
mujibu wa Mwansoko na wenzake (2006). Hatua hizo ni kama ifuatavyo:
1.
Hatua ya maandalizi. Hatua hii inahusisha mambo matatu ambayo ni:
a)
Kupitia tena sehemu muhimu za matini chanzi, kwa mfano; istilahi, majina ya
wahusika, majina ya kijiografia, maeneo au kauli zisizofasirika kirahisi.
b)
Kupata marejeleo ili kutafuta visawe vya kisemantiki
c) Kutafuta na kuandika visawe hivyo.
2. Hatua ya pili baada ya maandalizi ni
uhawilishaji (transferring/transference). Katika hatua hii mfasiri uhawilisha
ile taarifa kutoka kwenye matini chanzi kwenda kwenye matini lengwa, hapa
mfasiri anatakiwa kuzingatia sarufi ya lugha lengwa na lugha chanzi. mfano; “My
new car is broken”-langu jipya gari ni vunjika. Tafsiri ya Kiswahili sanifu
inapaswa kuwa “Gari langu jipya limeharibika” Uhawilishaji maana yake ni
kuhamisha maana, ujumbe nk. kutoka lugha chanzi kwenda lugha lengwa kwa
kuzingatia sarufi ya lugha lengwa, lengo la matini au mwandishi, umbo la
matini, mtindo nk. Mbinu ya tafsiri ambayo inatumika katika hatua hii ya
uhawilishaji ni tafsiri ya neno kwa neno.
3.
Hatua ya tatu ni kusawidi rasimu ya kwanza (drafting). Uhawilishaji wa visawe
kutoka lugha chanzi kwenda lugha lengwa unapokamilika kinachopatikana ni rasimu
ya kwanza ya tafsiri. Rasimu ya kwanza ya tafsiri inakuwa na dosari nyingi na
kwa hiyo haifai kupelekwa kwa mteja au hadhira. Badala yake rasimu ya kwanza
lazima ipitiwe tena upya na kurekebishwa au kudurusiwa/durusu (review) rasimu
(draft).
4.
Hatua ya nne ni kudurusu rasimu ya kwanza ili kuunda rasimu ya pili. Mfasiri
hupata fursa ya kwanza ya kuitathimini na kuifanyia marekebisho tafsiri yake
mwenyewe. Kazi ya kudurusu haipaswi kufanywa haraka. Wataalam wengine kama vile
Larson (1984) anasema rasimu ya kwanza ni lazima iachwe kwa muda wa wiki moja.
Udurusu unahusisha shughuli zifuatazo: · Kusahihisha makosa ya kisarufi, miundo
isiyoeleweka vizuri. · kunyoosha sehemu zenye tafsiri ya mzunguko na zenye
matumizi potofu ya visawe. Mfano; “He rarely visits me these days – Siku hizi
ni aghalabu-nadra sana yeye kunitembelea.” ·Kurekebisha sehemu zenye muunganiko
tenge/mbaya ambazo zinazuia mtiririko mzuri wa matini. Kuhakiki usahihi na
kukubalika kwa maana zinazowasilishwa katika matini lengwa. Hapa tunaangalia
kama kuna mambo yameongezwa, yamepunguzwa au yamepotoshwa/kubadilishwa.
·Kuhakiki kukubalika kwa lugha uliyotumia katika tafsiri yako kwa kuzingatia
umbo na mada ya matini chanzi. ·Kuona iwapo mada au ujumbe mkuu wa matini
chanzi unajitokeza waziwazi katika matini lengwa.
5.
Hatua ya tano ni kusomwa rasimu ya pili na mtu mwingine. Msomaji wa rasimu ya
pili anaweza kuwa mfasiri au shabiki wa tafsiri, mhakiki au mhariri wa tafsiri
anaweza kuwa mteja wa tafsiri husika au mtu mwingine yeyote unayemwamini. Namna
ya kumpa mtu akusomee rasimu: · Kumpa bila kumjulisha kwamba ni tafsiri ·
Unampa matini chanzi na matini lengwa ili alinganishe. Inapendekezwa kwamba mtu
huyo asome kwa sauti ili uweze kubaini mapungufu.
6.
Hatua ya sita ni kusawidi rasimu ya mwisho. Katika hatua hii mfasiri
atafanyiakazi maoni na mapendekezo ya msomaji ambaye alimpa kazi yake. Matokeo ya
kufanyiakazi maoni ya mteja hutupelekea kupata rasimu ya mwisho ambayo ndiyo
humfikia mteja, hadhira, wachapaji nk.
Shukrani.
JibuFutakazi nzuri.Shukrani.
JibuFutaKazi nzurii
JibuFutaSafi Sana kazi nzur
JibuFutaShukran hongera
JibuFutakazi nzuri ila tuongeze mawazo mengine kama mbinu za tafsiri na mengineyo yanayohusu tafsiri.
JibuFutaKazi nzuri, ina manufaa ajabu
JibuFutaJuu mwongozo ni muhimu xana
JibuFutaasante lakini jaribu kutupa mifano ya tafsiri kwenye nadharia
JibuFutaShukrani
JibuFutakazi nzuri lakini haina rejea
JibuFutaKazi nzuri
JibuFutaPongezi kwa kazi nzuri.. Jaribu kuandika kurasa ya marejeleo .
JibuFutaKazi nzuri. Nimeipenda
JibuFutaKazi nzuri sana. Hakikisha kwamba andiko lolote la kitaaluma linakuwa na marejeo kuwapa heshima wataalamu mbalimbali waliofanya kazi kubwa sana kweny uga wa kitaaluma.
JibuFutakazi nzuri sana
JibuFutaHeko! kwa kazi nzuri,ningependelea pia uongezee kwa kutuelezea Nadharia ya tafsiri kwa kuangalia
JibuFuta1.Isumu linganishi
2.Isimu jamii na
3.Mawasiliano katika tafsiri.
Shukran, ubarikiwe.
Kazi nzuri
JibuFutaAhsante mkuu.
JibuFutaKazi nzuri
JibuFutakazi nimeipenda mungu akuzidishie
JibuFutaSafi sana
JibuFutaKongole kwa kazi nzuri
JibuFutaKazi nzuri hii
JibuFutaNi zipi nadharia za tafsiri?
JibuFutaShukrani.
Kazi ni nzuri sana lakini haina marejeleo maana ake rukiiona tunasema umebuni mwenyewe kitu ambacho ndivyo sivyo
JibuFutaKazi nzuri kaka
JibuFutaInapendeza sana
JibuFutaUchi
Kazi nzuri lkn tungepata na sababu za Kuanzishwa kwa Tafsiri zisipungue 5
JibuFutaKazi safi ndugu
JibuFuta