USHAIRI
WA KISWAHILI
HAKI
1 Maisha haya jamani, kweli niipatashika
Maisha
kama majani, kweli yanapukutika
Maisha
yalo gizani, leo yaanasikika
Haki
yamtu jamani, hakika nipatashika.
2 Tuliishi kwaamani, tena kwakujiamini
Haki
zetu mikononi, wote tulizitieni
Lakini
wetu karani, leo twamzikeni
Haki
ya mtu jamani, hakika nipatashika.
3 Kila mnyonge nyumbani, wote
walifurahia
Swahibu
kwake moyoni, kwake alipigania
Amani
kwetu moyoni, wote tulisherekea
Haki
ya mtu jamani, hakika nipatashika.
4 Kichwa chake chahekima, busara zimesimama
Kelo za watu mapema, tayari kuzitazama
Waume
na kinamama, haki hawakulalama
Haki
ya mtu jamani, hakika nipatashika.
5 Tuliishi kwa matao, busara yake karani
Karani
wetu mtwao, sote twaweka kirini
Twakukumbuka
wanao, leo hii korokoroni
Haki
ya mtu jamani, hakika nipatashika.
6 Mungu ulo mbinguni, sikia hiki kilio
Mjalie
wetu karani, korokoroni kilio
Wote
tunamdhamini, twomba tena kwakilio
Haki
ya mtu jamani, hakika nipatashika.
NA
RICHARD, KASHINJE 0764711129
rkashinje@gmail.com
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni